• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Chamwino District Council
Chamwino District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadlili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Idara
      • Elimu Sekondari
      • Fedha
      • Mipango
      • Utawala na Utumishi
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Maji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo Umwagiliaji na Mazingira
      • Ardhi Maliaasili na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • TEHAMA
      • Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Agricultuer
    • Mifugo
    • Fishing
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha Uongozi na Mipango
      • Afya Elimu na Maji
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Ukimwi
      • Maadili
      • Ardhi
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyopitishwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu za Maombi
    • Sheria Ndogo
    • Mikakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

RC Dodoma Atembelea na Kukagua Miradi Ya Maendeleo Chamwino

Imewekwa: September 15th, 2025

Mkuu wa mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary S. Senyamule, jana tarehe 15 Septemba 2025 ametembelea na kukagua miradi mbalimbali ya maendeleo inayotekelezwa na serikali katika Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino ili kuimarisha na kuboresha huduma za kijamii kwa wananchi.

Miongoni mwa miradi iliyotembelewa ni mradi wa maji wa Miji 28 unaojengwa kwa Tsh. Bilioni 17. Mradi huo ambao una ujazo wa lita 500,000 una lengo la kuboresha upatikanaji wa maji safi na salama katika Mji wa Chamwino, ambapo utanufaisha kata 4, vijiji 7, vitongoji 48 na jumla ya wananchi 59,000.

Mradi huo unaotarajiwa kukamilika Mwezi Disemba mwaka huu, utaongeza upatikanaji wa maji safi na salama katika eneo la huduma la DUWASA kutoka 91% ya sasa hadi 100%. Aidha, unatarajiwa kuchochea maendeleo ya kiuchumi na kijamii katika Mji wa Chamwino.

Mradi mwingine uliotembelewa ni ujenzi wa kituo cha afya msanga ambao kwa awamu ya kwanza unahusisha ujenzi wa jengo la mama na mtoto, kichomea taka, vyoo vya wagonjwa na kuanzisha msingi wa jengo la upasuaji. Mradi huo ambao umeanza kutekelezwa mwaka huu 2025 baada ya Halmshauri ya Wilaya ya Chamwino kupokea Tsh. Milioni 250 kutoka serikali kuu, unatarijiwa kunufaisha wananchi 7,650 pale utakapokamilika.

Kadhalika, Mhe. Senyamule ametembelea ujenzi wa daraja la Nzali linalojengwa katika kata ya Chilonwa. Daraja hilo lina kina cha Mita 6.43, urefu wa Mita 60, na upana wa mita 11.4, pamoja na barabara za kuingilia zenye urefu wa kilomita 1.5 ambazo zitajengwa kwa kiwango cha changarawe. Daraja hilo ambalo ujenzi wake umefikia 65% linajengwa kwa Tsh. Bilioni 14.515 na linatarajiwa kukamilika  Mwishoni mwa Oktoba mwaka huu 2025.

Vilevile, Mhe. Senyamule ametembelea Shule ya Msingi Chalinze ambapo amekagua ujenzi wa vyumba viwili vya madarasa na matundu matatu ya vyoo ambayo yamejengwa shuleni hapo.

Hata hivyo, amehimiza wakandarasi wa miradi ambayo ujenzi wake unaendelea kuhakikisha kuwa wanakamilisha miradi hiyo kwa wakati ili ihudumie wananchi, huku akiwataka kuzingatia ubora.

Matangazo

  • MATOKEO DARASA LA SABA December 01, 2022
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KIDATO CHA KWANZA 2023. December 14, 2022
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2022 January 29, 2023
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI 2023 June 11, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC Dodoma Atembelea na Kukagua Miradi Ya Maendeleo Chamwino

    September 15, 2025
  • DAS Chamwino Apokea Ripoti Ya Utekelezaji Wa Mkataba Wa Lishe Kwa Robo Ya Nne Ya Mwaka Wa Fedha 2024/2025

    August 22, 2025
  • Chamwino Kuendesha Mafunzo Ya Siku Tatu Kwa Kamati Ya CAMFED Wilaya

    August 19, 2025
  • Vikundi 25 Vya Wanawake Na Vijana Vyanufaika Na Mkopo Wa Asilimia Kumi Wenye Thamani Ya Tsh. Milioni 132,850,200

    August 14, 2025
  • Angalia Zote

Video

UTEKELEZAJI, UKAMILISHAJI WA MRADI WA BOOST HALMASHAURI YA WILAYA YA CHAMWINO
Video Zaidi

Viunganifu vya Haraka

  • Mafanikio ya Miaka Miwili ya Mhe. Rais
  • Mapokezi ya Kidato cha Kwanza 2018
  • Historia ya Halmashauri
  • Dira na Dhima
  • Kituo cha Biashara
  • Kuonana na Mwenyekiti
  • Huduma za Watumishi
  • Maktaba ya Picha

Viunganishi Linganishi

  • Tanzania
  • PRo-RALG
  • Tovuti ya Wilaya ya Bahi
  • Parliament of Tanzania
  • Dodoma
  • Utumishi

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

Counter Widgets

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino

    Sanduku la posta: 1126 Dodoma

    Simu ya Mezani: 026 296 1511

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ded@chamwinodc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino. Haki zote Zimehifadhiwa.