• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Chamwino District Council
Chamwino District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadlili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Idara
      • Elimu Sekondari
      • Fedha
      • Mipango
      • Utawala na Utumishi
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Maji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo Umwagiliaji na Mazingira
      • Ardhi Maliaasili na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • TEHAMA
      • Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Agricultuer
    • Mifugo
    • Fishing
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha Uongozi na Mipango
      • Afya Elimu na Maji
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Ukimwi
      • Maadili
      • Ardhi
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyopitishwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu za Maombi
    • Sheria Ndogo
    • Mikakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Wasimamizi Wasaidizi Wa Uchaguzi Ngazi Ya Kata Wanolewa Chàmwino

Imewekwa: August 4th, 2025

Wasimamizi wasaidizi wa uchaguzi ngazi ya Kata katika majimbo ya Chamwino na Mvumi, Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino wameanza kupatiwa mafunzo ya siku 3 kuanzia leo tarehe 4 hadi 6 Agosti, 2025 kuhusu masuala mbalimbali ya Uchaguzi Mkuu wa Rais, Wabunge na Madiwani 2025.

Mafunzo hayo yenye lengo la kuwajengea uwezo Wasimamizi wasaidizi wa Uchaguzi ngazi ya Kata, yamefunguliwa na mgeni rasmi Bi. Prudence Kaaya ambaye pia ni Msimamizi wa Uchaguzi wa majimbo ya Chamwino na Mvumi na yanafanyika ili kuwafanya kutekeleza majukumu yao ya kusimamia hatua mbalimbali za Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2025.

Akizungumza wakati wa ufunguzi, Bi Kaaya amewapongeza washiriki kwa kuteuliwa na kuaminiwa kutekeleza na kusimamia shughuli za uchaguzi Mkuu wa Rais, wabunge na madiwani utakaofanyika Oktoba 29, 2025.

Halikadhalika, Ndg. Kaaya amewaaasa Wasimamizi wasaidizi wa uchaguzi ngazi ya kata kusoma katiba, sheria, kanuni, taratibu, miongozo na  maelekezo yote yanayotolewa na Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi kwani Tume hiyo ndiyo yenye mamlaka ya kusimamia na kuratibu shughuli za Uchaguzi Mkuu wakati wa utekelezaji wa shughuli zao za Uchaguzi.

“Nachukua nafasi hii kuwaasa pamoja na uzoefu ambao baadhi yenu mpo nao katika kutekeleza shughuli za uchaguzi kusoma katiba, sheria, kanuni, taratibu na miongozo pia fuateni maelekezo mbalimbali yanayotolewa na Tume katika kutekeleza shughuli za uchaguzi”. Alisema Bi. Kaaya

Pia amewahimiza kuzingatia kuvishirikisha vyama vyote vya siasa vyenye usajili kamili katika hatua zote kwa kuzingatia matakwa ya kikatiba, sheria, kanuni na maelekezo mbalimbali ya Tume, pamoja na kujiepusha kuwa vyanzo vya malalamiko kutoka kwa vyama vya siasa na wadau wa uchaguzi.

Matangazo

  • MATOKEO DARASA LA SABA December 01, 2022
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KIDATO CHA KWANZA 2023. December 14, 2022
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2022 January 29, 2023
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI 2023 June 11, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • Vikundi 25 Vya Wanawake Na Vijana Vyanufaika Na Mkopo Wa Asilimia Kumi Wenye Thamani Ya Tsh. Milioni 132,850,200

    August 14, 2025
  • Zahanati Tano Chamwino Zapatiwa Vifaa Tiba Vyenye Thamani Ya Zaidi Ya Milioni Kumi

    August 14, 2025
  • Shule za Msingi Na Sekondari Chamwino Zajengewa Vizimba Vya kunawia Mikono

    August 13, 2025
  • Kamishina Tume Huru Ya Uchaguzi Atembelea Mafunzo Ya Wasimamizi Wasaidizi Wa Uchaguzi Ngazi ya Kata Wilayani Chamwino

    August 06, 2025
  • Angalia Zote

Video

UTEKELEZAJI, UKAMILISHAJI WA MRADI WA BOOST HALMASHAURI YA WILAYA YA CHAMWINO
Video Zaidi

Viunganifu vya Haraka

  • Mafanikio ya Miaka Miwili ya Mhe. Rais
  • Mapokezi ya Kidato cha Kwanza 2018
  • Historia ya Halmashauri
  • Dira na Dhima
  • Kituo cha Biashara
  • Kuonana na Mwenyekiti
  • Huduma za Watumishi
  • Maktaba ya Picha

Viunganishi Linganishi

  • Tanzania
  • PRo-RALG
  • Tovuti ya Wilaya ya Bahi
  • Parliament of Tanzania
  • Dodoma
  • Utumishi

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

Counter Widgets

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino

    Sanduku la posta: 1126 Dodoma

    Simu ya Mezani: 026 296 1511

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ded@chamwinodc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino. Haki zote Zimehifadhiwa.