Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Chamwino Mhe. Edson Sweti amewashukuru wahe. Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino pamoja na Wakuu wa Idara/Vitengo kwa ushirikiano mzuri waliompatia kwa kipindi chote cha miaka mitano cha uongozi wake.
Ameyasema hayo kwenye mkutamo maalum wa Baraza la Madiwani uliofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa Halmashauri Juni 18, 2025 ambapo alitumia fursa hiyo kuwaaga kutokana na mabaraza yoteya Madiwani nchini kuvunjwa ifikapo Juni 20, 2025 kwa ajili ya kupisha uchaguzi mkuu.
" Nitumie fursa hii kuwashukuru kwa ushirikiano mlioniopatia ninyi Waheshimiwa Madiwani wote pamoja na wakuu Waidara/Vitengo kwa kipindi chote cha miaka mitano cha uongozi wangu. Haikuwa kazi rahisi lakini mliweza kuniamini na kunipa ushirikiano mzuri, pengine wahe. Madiwani mngeweza kuazimia na kuniondoa kwenye uongozi huo lakini hamkufanya hivyo. Ninawashukuru sana na nawatakia kila la heri kwa wale mtakaoingia tena kwenye kinyanga'anyiro cha uchaguzi." Alisema Mhe. Mwenyekiti.
Naye kaimu Mkurugenzi wa Halmashaurindugu Godfrey Mnyamale amewashukuru kwa uongozi wao mzuri nakueleza kuwa huo ndiyo uliyowezesha mafanikio na maendeleo yaliyopatikana ndani ya Halmashauri yetu. Naye pia aliwatakia heri kwa kipindi hiki wanapoondoka.
Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino
Sanduku la posta: 1126 Dodoma
Simu ya Mezani: 026 296 1511
Simu ya Mkononi:
Barua Pepe: ded@chamwinodc.go.tz
Hakimiliki©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino. Haki zote Zimehifadhiwa.