Mkuu wa Wilaya ya Chamwino, Mhe. Janeth Mayanja, leo Februari 11, 2026 amepokea taarifa ya utekelezaji wa mkataba wa lishe kwa robo ya pili ya mwaka wa fedha 2025/2026, kwenye kikao cha tathimini kilichofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa ofisi ya Mkuu wa Wilaya.
Kikao hicho ambacho kimejumuisha wataalamu kutoka Halmashauri, watendaji wa Vijiji na Kata, na wadau wa lishe, pamoja na kujaadili taarifa ya utekelezaji wa mkataba wa lishe, kimeweka maazimio mbalimbali yanayolenga kuimarisha hali ya lishe katika wilaya ya Chamwino hasa katika Vijiji na Kata ambazo hazifanyi vizuri.
Moja ya maazimio hayo, ni kufanya suala la lishe kuwa ajenda ya kudumu ili kuwezesha utoaji endelevu wa elimu ya lishe. Vilevile, kuweka mikakati thabiti itakayowezesha upatikanaji wa chakula kwa wanafunzi wote wa shule za msingi na sekondari, pamoja na kuongeza upatikanaji wa chakula kilichoongezwa virutubishi.
Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino
Sanduku la posta: 1126 Dodoma
Simu ya Mezani: 026 296 1511
Simu ya Mkononi:
Barua Pepe: ded@chamwinodc.go.tz
Hakimiliki©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino. Haki zote Zimehifadhiwa.