Baraza la Madiwani katika Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino, leo Februari 12, 2026 limefanya mkutano wa robo ya pili ya mwaka wa fedha 2025/2026 katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ambapo limepokea na kujadili taarifa za utekelezaji za Kata kwa kipindi hicho cha mwezi Oktoba – Disemba 2025.
Katika mkutano huo Madiwani wamewasilisha taarifa zilizoainisha mafanikio yaliyofikiwa na kubainisha changamoto mbalimbali zinzohitaji utatuzi katika kata zao.
Mafanikio yaliyoelezewa ni pamoja na kuimarika kwa upatikanaji wa huduma za kijamii, pamoja na uwezeshaji wa wananchi kiuchumi kupitia mikopo ya asilimia kumi inayotolewa na Halmashauri kwa vikundi vya wajasiriamali vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu.
Imeelezwa kuwa katika kipindi hicho, Kata mbalimbali zimejengewa shule mpya za msingi na sekondari na ukarabati wa miundimbinu ya shule za zamani, ujenzi wa nyumba za walimu, ujenzi wa vituo vya kutolea huduma za afya, na ongezeko la watumishi katika sekta za afya, elimu na maendeleo ya jamii, waliotokana na ajira mpya zilizotolewa na serikali.
Mafanikio mengine yaliyoolezwa ni kuimarika kwa ufaulu wa wanafunzi katika shuke za msingi na sekondari, uwekaji wa miundombinu ya TEHAMA katika shule za msingi na sekondari, ujenzi wa chuo cha VETA, ujenzi wa barabara na madaraja, kuimarika kwa ulinzi na usalama, ujenzi wa minara ya simu, ongezeko katika utoaji wa mikopo ya asilimia kumi, pamoja na kuongezeka kwa usambazaji wa umeme na maji safi na salama.
Mbali na mafanikio hayo, madiwani wameeleza changamoto mbalimbali zinazokabili kata zao, ikiwa ni pamoja na kuharibika kwa miundombinu ya barabara na maji safi kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha na wameomba hatua mahususi zichukuliwe kutatua changamoto hizo.
Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino
Sanduku la posta: 1126 Dodoma
Simu ya Mezani: 026 296 1511
Simu ya Mkononi:
Barua Pepe: ded@chamwinodc.go.tz
Hakimiliki©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino. Haki zote Zimehifadhiwa.